Wanafunzi 20 wa timu ya mpira wa miguu ya Chuo Kikuu cha Buea, magharibi mwa Cameroon waliotekwa nyara juzi wameachiliwa huru jana usiku baada ya kupigwa sana.
Kocha wa timu hiyo Bw. Nicolas Asongu amesema, wanafunzi hao waliachiliwa huru jana baada ya saa 2 jioni, lakini hawakuwa na afya nzuri. Amesema baadhi ya wanafunzi wamejeruhiwa, na baadhi yao wameathirika kisaikolojia na wanahitaji msaada, huku wengine wamelazwa hospitali wakipatiwa matibabu.
Mpaka sasa hakuna mtu ama kundi lililokiri kuwajibika na utekaji nyara huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |