Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema nchi hiyo itawasilisha waraka kwa Umoja wa Mataifa kuhusu suala la Marekani kutambua mamlaka ya Israel kwenye milima ya Golan .
Rais Ergogan alipohojiwa na Shirika la Utangazaji la TGRT Haber alisema kauli ya rais Donald Trump wa Marekani kuhusu milima ya Golan ni zawadi kwa waziri mkuu wa Israel Bw. Benjamin Netanyahu kabla ya uchaguzi mkuu mwezi ujao.
Alhamisi wiki iliyopita Rais Trump alisema ni wakati kwa Marekani kutambua mamlaka ya Israel kwa pande zote kuhusu milima ya Golan, na maneno yake yalisababisha upinzani na laumu duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |