Waziri mkuu wa Palestina Bw. Mohammad Ishtaye ametangaza kuwa amemaliza mazungumzo na Chama cha PLO kuhusu uundaji wa serikali ya umoja.
Amesema mazungumzo yamefanyika kwa muda wa wiki mbili, na mbali na PLO pia amefanya mikutano na wajumbe wa mashirikisho ya umma, sekta binafsi na mabaraza ya madiwani. Ameongeza kuwa mazungumzo yamefanyika katika hali chanya, na sasa anasubiri majibu ya makundi mbalimbali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |