• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Michuano ya mwisho ya kufuzu AFCON 2019: Burundi, DRC wawafuata Uganda na Kenya, Stars yaweka rekodi baada ya miaka 39.

    (GMT+08:00) 2019-03-25 10:12:56

    Timu ya taifa ya Burundi kwa mara ya kwanza katika historia imefanikiwa kuweka rekodi mpya katika soka lake baada ya kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika AFCON 2019 zitakazofanyika nchini Misri Juni mwaka huu.

    Burundi imefuzu kucheza michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya mchezo wao kumalizika kwa sare ya kufungana goli 1-1. DRC nao wamefanikiwa kufuzu baada ya kuipiga Liberia goli 1-0 katika uwanja wa Tata Raphael mjini Kinshasa. Kimbembe kilikuwa jana kwa Tanzania, kwa mara ya kwanza baada ya miaka 39 timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars wameunagana na wenzao wa Afrika Mashariki kufuzu michuano hiyo baada ya kuichapa Uganda Cranes mabao 3-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

    kwa mara ya kwanza Afrika Mashariki inaingiza mataifa matano (Uganda, Kenya, Tanzania, Burundi na DRC) katika fainali za AFCON .

    Mataifa mengine 19 ambayo tayari yamefuzu ni Angola, Madagascar, Tunisia, Misri, Senegal, Nigeria, Mali, Morocco, Algeria, Ivory Coast, Mauritania, Guinea, Ghana, Guinea Bissau, Namibia na Cameroon

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako