Mwakinyo amemaliza kilichompeleka Kenya kwa kupambana na bondia wa Argentina Sergio Gonzalez ambapo mtanzania huyu amechukua ushindi kwa kumpiga Sergio kwa K.O kwenye round ya 5 ya mchezo.
Pambano hilo lisilo la ubingwa, lililopigwa kwenye ukumbi wa KICC jijini Nairobi Kenya.
Kwa upande wa wanawake, Iron First wa Kenya Zarika Fatuma ametetea taji lake la ubingwa wa Super Bantam alipomchakaza bondia toka Zambia Catherine Phiri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |