• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Michuano ya kufuzu mataifa ya Ulaya (EURO 2020): Mambo ni Bam Bam

    (GMT+08:00) 2019-03-25 10:14:29
    Wikiendi hii iliyomalizika jana ilikuwa na mshikemshike kwa michuano mbalimbali duniani, michuano ya kufuzu mataifa ya ulaya EURO 2020 mambo ni Bam Bam, Timu ya taifa ya Uingereza imeipiga Jamhuri ya Czech bao 5-0 katika kundi A, mchezo uliopigwa uwanjani Wembley Uingereza.

    Kundi B, Luxembourg imeifunga Lithuania goli 2-1, huku Ureno ikitoka sare na Ukraine. Kundi D, Uswisi imeibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Georgia, na kundi H, Uturuki imeifunga Albania bao 2-0, Iceland wameibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Andorra na Ufaransa ikiichakaza Moldova mabao 4-1.

    Michuano mingine imepigwa jana na usiku wa kuamkia leo, Kundi D Ireland imeifunga Gibraltar goli 1-0, huku Group E, Wales imetoka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Slovakia. Matokeo ya kundi F, Malta wameifunga Kisiwa cha Faroe goli 2-1, nayo Sweden wakiibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Romania, na Uhispania imeshinda 2-1 dhidi ya Norway.

    Katika kundi I, Kazakhstan imekubali kichapo cha 4-0 toka kwa Urusi, na kundi H, Italia imeipiga Finland 2-0, Greece wameipiga Liechtenstein 2-0.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako