Hayo yalisemwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dk Leonard Chamuriho katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Sekta ya Uchukuzi ambao ulilenga kupitia na kupitisha Bajeti ya Sekta ya Uchukuzi fungu namba 62.
Chamuriho alisema bajeti hiyo itatumika kutekeleza miradi mingi mikubwa itakayokuwa inaendelea kama vile mradi wa reli ya kisasa kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro.
Aidha alisema mradi mwingine ambao utafadhiliwa na fedha hizo ni ujenzi wa reli hiyo kipande cha Morogoro hadi Makutupora chenye urefu wa kilomita 422.
Aidha alisema wanaendelea kuimarisha shirika la ndege Tanzania (ATCL) na wataendelea kukamilisha mipango iliyopangwa awali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |