Rais wa zamani wa Brazil Michel Temer na wasaidizi wake muhimu saba wameachiwa huru kutoka gerezani kufuatia kukamatwa kwao wiki iliyopita kwa makosa ya ufisadi. Bw. Temer aliachiwa huru na jaji Antonio Athie siku mbili kabla ya jopo la majaji kutarajiwa kutoa uamuzi kuhusu ombi lililotolewa na timu ya utetezi ya Bw. Temer. Bw. Athie amesema baada ya kupitia kesi hiyo kwa makini, amethibitisha kuwa hakuna sababu halali ya kusubiri siku nyingine mbili kuhusu kuachiwa huru. Ameongeza kuwa kwa mujibu wa Katiba, mtuhumiwa ana haki ya kuwa huru anaposubiri kesi yake kufunguliwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |