Ameongeza kuwa alama ya ubora pia humsaidia mzalishaji kupanua masoko ya bidhaa zake nje ya nchi na ni wazi kuwa hatua hiyo ni ya kujivunia sana kama mzalishaji na kama taifa kupanuka kwa masoko ya kikanda na kimataifa kutasaidia kuongeza fedha za kigeni na hatimaye kusaidia kukuza uchumi.
Alifafanua kuwa hali hiyo itasaidia kufikiwa kwa azima ya taifa ya kujenga uchumi wa kati unaotegemea uzalishaji wa viwandani ifikapo mwaka 2025.
Aliwataka wazalishaji waliopatiwa leseni hizo kuzingatia masharti yake na kuwa waadilifu katika uzalishaji wao, ili kuhakikisha wanaendelea kuzalisha bidhaa zinazokidhi matakwa ya viwango wakati wote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |