• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: EU yaipiga faini kampuni ya NIKE

    (GMT+08:00) 2019-03-27 08:30:28
    Mamlaka ya ushindani ya Jumuiya ya Ulaya (EU) imeipiga faini ya dola 14 milioni za marekani kampuni kubwa duniani ya kutengeneza vifaa vya michezo ya Nike kwa kuweka masharti ya mauzo ya jezi na skafu za klabu kubwa za soka nje ya nchi zao.

    Kwa mujibu wa kamisheni ya Ulaya, Nike iliingia mikataba isiyo halali kisheria kwa vifaa kwa klabu za FC Barcelona, Manchester United, Juventus, Inter Milan na AS Roma pamoja na timu za taifa wakiwemo mabingwa wa soka duniani Ufaransa.

    Kiongozi wa kamisheni hiyo Margrethe Vestager amebainisha kuwa, mashabiki wa soka hupenda kununua vifaa mbalimbali vilivyowekwa nembo za klabu zao ikiwemo skafu, jezi, Nike ilizuia aina hiyo ya bidhaa kwenye nchi nyingine na kusababisha mashabiki kutokuwa na uwanja mpana wa kuchagua ama kununua kwa bei kubwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako