Waasi wasiopungua 15 wa kundi la Houthi wameuawa na wengine kadhaa wamejeruhiwa katika mapambano na wanajeshi wa serikali mkoani Saada, kaskazini mwa Yemen. Afisa habari wa kikosi cha brigedi ya 102 Bw. Faiz al-Sadi ameeleza kuwa mapambano hayo yaliibuka wakati wanajeshi hao walipozuia shambulizi lililofanywa na waasi katika maeneo ya kijeshi, na pia kuna wanajeshi watatu waliojeruhiwa katika mapambano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |