Watu sita wamefariki dunia papo hapo na wengine watano wamejeruhiwa vibaya katika ajali ya barabarani iliyotokea kaskazini mwa Uganda. Msemaji wa polisi ya eneo la North Kyoga Bw. David Ongom amesema dereva wa gari aina ya Toyota Noah alijaribu kuipita teksi kwa mwendo kasi na kuigonga kwa nyuma kabla ya kusababisha ajali katika barabara inayotoka Dokolo hadi Amolatar. Magari hayo mawili yalikuwa yakiwapelekea abiria kupanda meli.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |