Makamu rais wa Tanzania Bibi Samia Suluhu Hassan amehimiza nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC kuwekeza kwenye teknolojia ya kidijitali ili kuharakisha utimizaji wa lengo la Umoja wa Mataifa la maendeleo endelevu.
Bibi Hassan amesema, teknolojia ya kidijitali ya afya itasaidia kuboresha huduma za afya za kikanda na kuondoa umaskini. Pia amesema, Tanzania imeanza kutumia teknolojia hiyo kusaidia wizara ya afya kufahamu usafirishaji na matumizi ya dawa.
Bibi Hassan amesema, hivi sasa, pendekezo hilo linahitaji nguvukazi zaidi na uungaji mkono wa kifedha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |