• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kamati ya Bunge kuhusu Kilimo yataka Wizara ya Biashra kusitisha uagizaji maziwa kutoka nje

    (GMT+08:00) 2019-03-28 19:52:23
    Kamati ya Bunge kuhusu kilimo nchini Kenya imeiwekea mguu Wizara ya biashara na kuitaka kusitisha uagizaji wa maziwa kutoka nchi za nje.ikidai kuwa uagizaji huo unawaathiri wafugaji ng'ombe wa maziwa.

    Mwenyekiti wa kamati ya kilimo Bungeni,Emmanuel Wangwe jana alisema serikali haifai kuendelea kuagiza kugiza bidhaa hiyo ilhali kiwango cha maziwa kinachozalishwa nchini kinatosehleza mahitaji ya soko.

    Aidha Wangwe,amabye pia ni mbunge wa Navakholo alisema Kenya inazalisha kilo 5.7 bilioni za maziwa kila mwaka ilhali hitaji la kitaifa ni kilo 5.2 bilioni pekee.

    Aliongeza kuwa mwenendo huo wa serikali wa kuendelea kuagiza maziwa kutoka nje unawaumiza wakulima na unapasa kusitishwa mara moja.

    Alisema uagizaji huo umechangia kupungua kwa bei ambayo wafugaji huuza maziwa yao kwa kampuni za kutayarisha maziwa kutoka Sh42 hadi Sh28 kwa lita moja.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako