Nyota huyo alitumia fursa hiyo kucheza na watoto wakimbizi kusakata kabumbu, huku yeye akicheza nafasi ya golikipa.
Kuhusiana na ziara hiyo, Eto'o amesema, anataka watoto wa wakimbizi kutoka Afrika ya kati wajisikie vizuri huku lengo lake kubwa ni kuona watoto hao wanaambatana na wazazi wao kurejea makwao katika hali ya usalama.
Eto'o alishindwa kujizuia kutokwa machozi baada ya kushuhudia vipaji mbalimbali vya michezo walivyonavyo watoto hao na kuahidi kuwasaidia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |