Magwiji wa klabu ya Manchester United sasa roho kwatu baada ya Ole Gunnar Solskjaer kukabidhiwa rasmi mikoba kufundisha timu hiyo kwa mkataba wa miaka mitatu. Hilo limekuja baada ya kuingoza timu hiyo ikipoteza mara moja tu katika mechi 13 ilizocheza kwenye ligi kuu ya Uingereza (EPL).