Waziri mkuu wa Ethiopia Bw. Abiy Ahmed amepongeza uhusiano imara wa kiuchumi kati ya nchi hiyo na China.
Bw. Ahmed amesema hayo katika mkutano na wanahabari uliofanyika katika ofisi yake huko Addis Ababa, huku akiongeza kuwa uhusiano imara wa kiuchumi kati ya nchi hiyo na China umeisaidia Ethiopia kutimiza ukuaji wa kiwango cha asilimia zaidi ya kumi kwa miaka zaidi ya kumi.
Pia amesema, uhusiano kati ya nchi hizo mbili umekuwa imara zaidi, na China imekuwa na itaendelea kuwa muungaji mkono mkubwa wa Ethiopia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |