Rais Xi Jinping wa China na mke wake Bibi Peng Liyuan wakiwa ziarani nchini Italia, Monaco na Ufaransa kuanzia Machi 21 hadi 26 .
Kwa Bibi Peng Liyuan ziara hiyo imebeba mambo matatu.
Kwanza ni shughuli za mambo ya taifa
Kuandamana na rais Xi Jinping kuhudhuria shughuli za ziara ya kitaifa, zikiwemo sherehe ya makaribisho, kutoa hotuba na kuhudhuria tafrija ya makaribisho.
Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa na mke wake hawakuweza kusubiri kwa siku nyingi zaidi kukutana na rais Xi na Bibi Peng huko Paris, walitangulia kwenda Nice wakati wa wikiendi.
Si kawaida kufanya sherehe ya makaribisho chini ya Triumphal arch. Raia wengi walikuja kutazama sherehe hiyo kukiwa na upepo mkubwa.
Paris, tafrija ya kusherehekea, waliendelea kuzungumza zaidi.
Pili: shughuli za ufadhili
Bibi Peng Liyuan ana wajibu wa aina mbili wa kimataifa
Baadhi ya watu wanamwita balozi—balozi wa Umoja wa Mataifa wa Kifua Kikuu na UKIMWI
Na wengine wanamwita mjumbe maalumu—mjumbe maalumu wa UNESCO wa kuhimiza elimu ya watoto wa kike na wanawake
Mara hii, Bibi Peng Liyuan alihudhuria sherehe ya utoaji tuzo maalumu ya elimu ya watoto wa kike na wanawake ya UNESCO iliyofanyika kwenye makao makuu yake mjini Paris.
Na Tatu: utamaduni na sanaa
Kuzingatia taaluma ya Bibi Peng Liyuan, nchi husika huenda zikandaa shughuli za utamaduni na sanaa.
Nchini Monaco, mke wa Prince Albert II amemwalika mwanamuziki wa China kupiga violin.
Nchini Italia, rais Sergio Mattarella wa Italia ameandaa tafrija na kuwalika mwimbaji maalumu Andrea Bocelli.
Nchini Ufaransa, Bibi Peng Liyuan ametembelea Opera ya Paris
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |