Wanajeshi wasiopungua 13 na makumi ya waasi kutoka kundi la Houthi wameuawa jana kwenye mapambano yaliyotokea mkoani Dhalea, kusini mwa Yemen.
Mapambano hayo yalitokea baada ya waasi hao kudhibiti ngome zilizoko kaskazini mwa Dhalea siku tatu zilizopita, umbali wa kilomita 245 kutoka kusini mwa mji mkuu Sanaa. Vikosi vya serikali vimetwaa tena ngome hizo kutoka kwa waasi baada ya mapambano hayo yaliyosababisha vifo na majeruhi wengi.
Wakati huo huo, mjumbe wa kundi la Houthi Mohammed Abdulsalam jana alikutana na mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa Bw. Martin Griffiths nchini Oman, ambako wamejadiliana kuhusu njia ya kumaliza mvutano kwenye mchakato wa kutimiza amani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |