Watu wasiopungua 25 wamefariki na wengine 400 wamejeruhiwa baada ya dhoruba kuzikumba wilaya mbili nchini Nepal. Waziri mkuu wa Nepal Bw. Sharma Oli amethibitisha kutokea kwa maafa hayo na kutoa salamu za rambirambi kwa familia za wafiwa. Amesema serikali imetuma wafanyakazi wa usalama kufanya operesheni za uokoaji katika maeneo yaliyoathiriwa na maafa hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |