Mameneja wa mfuko wa pensheni wa Kenya na Marekani wanatarajiwa kukutana mjini Nairobi leo, ili kutathmini uwezo na fursa za uwekezaji katika miundombinu nchini Kenya. Benki ya Dunia imesema katika mkutano huu wa siku tatu Jumuiya ya Uwekezaji wa Mfuko wa Pensheni ya Kenya KEPFIC itakutana na wawakilishi 30 wa Mifuko Mikubwa ya Usimamizi wa Pensheni na Mali ya Marekani ili kujadili fursa za uwekezaji na jumuiya hiyo pamoja na uanachama wake wenye mameneja 12 wa mfuko wa Kenya, ambao kwa sasa unashughulikia mali zenye thamani ya shilingi bilioni 200 za Kenya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |