Wachezaji wanne Haron hakava, Shafik Batambuze, Jacques Tuyisenge na Ernest Wendo wa timu ya Gor Mahia ya Kenya, watakosa mechi baina ya timu yao itakapomenyana na Berkane ya Morocco kwenye mchezo wa robo fainali ya kombe la Shirikisho mwezi ujao.
Beki Shakava atakosa mechi ya April 7 pekee kutokana na kuwa na kadi mbili za njano katika mechi tofauti za mashindano hayo, wengine waliosalia watakosa mechi ya kwanza na ya marudiano itakayopigwa nchini Morocco April 14.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |