Jeshi la anga la Nigeria limesema kikosi chake maalumu kimewaua watu watano wenye silaha wakati linazuia mashambulizi kwenye vijiji viwili vilivyopo katika jimbo la Zamfara, kaskazini magharibi mwa nchi hiyo. Duru za kijeshi zimesema washambuliaji wengine wengi wamekimbilia msituni wakiwa na majeraha ya risasi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |