Rais Abdelazizi Bouteflika wa Algeria amesema atajiuzulu kabla ya muhula wake kumalizika tarehe 28 Aprili. Taarifa iliyotolewa na ikulu ya Algeria imesema rais Bouteflika atafanya maamuzi muhimu kulingana na katiba ili kuhakikisha mwendelezo wa kazi za taasisi za kitaifa wakati wa mchakato wa mpito utakaoanza siku atakayojiuzulu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |