• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • RIADHA: Kenya, Ethiopia na Uganda zang'ara mbio za nyika nchini Denmark

    (GMT+08:00) 2019-04-02 09:11:19

    Wanariadha kutoka mataifa ya Kenya, Ethiopia na Uganda wameng'ara katika mbio za nyika za dunia zilizomalizika mwishoni mwa wikiendi jijini Aarus nchini Denmark.

    Kutoka Uganda Joshua Cheptegei ameshinda medali ya dhahabu katika mbio hizo kwa upande wa watu wazima kwa kutumia dakika 31:40 akifuatiwa na mwenzake kutoka nchi hiyo hiyo, Jacob Kiplimo, aliyetumia dakika 31: 44, Geoffrey Kipsang Kamworor wa Kenya, ambaye ndiye alikuwa anashikilia taji hilo, ameambulia nafasi ya tatu.

    Kwa upande wa wanawake, Mkenya Hellen Obiri, ameibuka mshindi kwa kutumia dakika 36:14 huku Dera Didam amekamata nafasi ya pili kwa kutumia dakika 36:16, nafasi ya tatu ikichukuliwa na Letesenbet Gidey wa Ethiopia.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako