Rais Donald Trump wa Marekani ameonya kuwa yuko tayari kwa asilimia 100 kufunga mpaka wa kusini kama hakuna makubaliano kufikiwa na bunge kuhusu mageuzi ya uhamiaji. Amesema Marekani imechoshwa kuwashughulikia wahamiaji haramu na hili ni jambo lisilo la haki. Amekosoa nchi za Amerika ya Kati za Honduras, Guatemala na El Salvador kwa kushindwa kukagua wahamiaji wanaoingia Marekani, akitishia kusimamisha msaada kwa nchi hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |