Mapigano makali na matumizi ya mizinga yameibuka kati ya wanajeshi wa serikali ya Yemen na waasi wa Houthi katika pembezoni mwa kusini mashariki mjini Hodeidah wakati Umoja wa Mataifa unafanya juhudi za kiamani kudumisha makubaliano ya usimamishaji vita. Mpaka sasa hakuna vifo au majeruhi kuripotiwa. Hali inazidi kuwa mbaya saa kadhaa baada ya Shirika la Mpango wa Chakula Duniani kuzuiliwa kufikia vinu vya mji huo kuweka dawa kwenye tani elfu 51 za ngano ili zisiharibike. Umoja wa Mataifa umeonya kuhusu shambulizi dhidi ya msaada wa chakula, linaloweza kuhatarisha makazi ya mamilioni ya Wayemen.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |