• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya yaanzisha sheria kuyasaidia makampuni madogo na yenye ukubwa wa kati kupata mkopo

    (GMT+08:00) 2019-04-03 09:33:35

    Kenya inapanga kuweka mfumo wa kisheria na udhibiti unaoyahamasisha mabenki kupanua mikopo kwa makampuni madogo na yenye ukubwa kati (SME).

    Waziri wa Viwanda, Biashara na Ushirika Bw. Peter Munya amesema makampuni madogo hayana sifa ya kupata mikopo ya benki kwa sababu yanaonekana kuwa na hatari kubwa ya kushindwa kulipa, hivyo katika miezi minne ijayo sheria itaanzishwa kwa mpango wa dhamana ya mikopo ambayo serikali itahakikisha mikopo inatolewa kwa mashirika hayo.

    Bw. Munya amesema hayo kwenye mkutano wa 16 wa Mfuko wa Binafsi wa Equity na shirika la uwekezaji wa hatari.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako