Mabingwa wa voliboli wa Kenya, General Service Unit (GSU) wamepoteza mchezo wao dhidi ya Asari kutoka Libya katika mechi yao ya kwanza kwa seti 3-2 ya klabu bingwa Afrika iliyoanza jijini Cairo nchini Misri, Jumatatu.
Akizingumza kutokea Misri baada ya mechi hiyo ya Kundi D, Kocha mkuu wa GSU Gideon Tarus ameeleza kuwa walizidiwa kimchezo na Asaria lakini wanajipanga vilivyo kushinda mchezo wao wa pili dhidi ya Nemo Stars kutoka Uganda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |