Shirika la uvuvi katika ziwa Victoria nchini Uganda limesema kuwa wavuvi walio na leseni ya kuvua samaki aina ya Nile Perch hawafai kuvua aina nyingine.
Katibu wa shirika hilo Dk. Shigalla Bassanda Mahongo uamuzi huo pia umekubaliwa nchi zote tatu zinazopakana na ziwa Vitoria.
Alisema boti zote za wavua samaki zitakuwa na nembo na nambari maalum inayoonyesha nchi inakotokea.
Amesema hatua hiyo italinda baadhi ya aina ya samaki ambao wanavuliwa sana.
Mkurungezi wa sekta ya uvuvi nchini Uganda Dk. Rhoda Tumwebaze, amesema tayari agizo hilo limeanza kutekelezwa likiendshwa na maafisa wa wizara ya mifugo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |