• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa Misri na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa wajadili masuala ya kikanda na vita dhidi ya ugaidi

    (GMT+08:00) 2019-04-04 09:10:25

    Rais Abdel-Fattah al-Sisi wa Misri amefanya mazungumzo na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres aliyefanya ziara nchini humo kuhusu maswala mbalimbali ya kikanda na juhudi zinazoendelea za kupambana na ugaidi. Rais Sisi na Bw. Guterres wamejadili maendeleo ya hivi karibuni katika eneo la Mashariki ya Kati haswa hali ya Libya, Syria na Yemen, nchi zinazokabiliwa na machafuko. Bw. Guterres ameahidi kuwa Umoja wa Mataifa unapenda kushirikiana zaidi na Misri katika kulinda amani na usalama katika eneo la Mashariki ya Kati. Bw. Guterres anatarajiwa kwenda Libya baada ya ziara yake mjini Cairo kabla ya mkutano wa kitaifa unaofadhiliwa na Umoja wa Mataifa, unaolenga kuandaa mazingira kwa ajili ya uchaguzi, ili kusaidia kumaliza mgogoro uliodumu kwa miaka mingi nchini Libya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako