Shirika la televisheni ya kulipia la China StarTimes, limesema litazingatia maudhui ya kikanda ili kuongeza idadi ya watazamaji wake barani Afrika.
Meneja Masoko mpya wa shirika hilo Bw. Aldrine Nsubuga amehimiza kuongeza maudhui ya kienyeji katika vipindi vyake ili kuongeza idadi ya watazamaji wake katika nchi ambazo shirika hilo la China limeshaanzisha shughuli.
Bw. Nsubuga aliyejiunga na ofisi ya kikanda ya StarTimes huko Nairobi kutoka Uganda wiki mbili zilizopita amesema, maudhui ya kienyeji ni muhimu kwa ukuaji wa kituo cha televisheni. Utafiti umeonesha kuwa nne kati ya cheneli saba zinazotazamwa zaidi, ni mitandao ya televisheni inayotengenezwa huko.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |