Matumaini ya ubingwa wa Tanzania bara yamezidi kufifia, Yanga SC baada ya kulazimisha sare ya kufungana 1-1 na wenyeji Ndanda FC katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania bara jioni ya jana uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Sare hiyo imeiongezea pointi moja Yanga SC na kufikisha 68 baada ya kucheza mechi 29, sasa wakiizidi kwa pointi sita tu Azam FC wanaofuatia katika nafasi ya pili, lakini furaha zaidi ni kwa mabingwa watetezi, Simba walio nafasi ya tatu na pointi zao 57 za mechi 22 tu kwani upinzani unazidi kupungua kwenye mbio za taji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |