Vikosi vya Iraq vimewakamata wapiganaji wengi wa kundi la IS akiwemo kiongozi maarufu wa kundi hilo anayesemekana kuwa ni mshirika wa karibu wa kiongozi wa kundi hilo Abu Bakr al-Baghdadi katika mkoa wa Diyala, mashariki mwa nchi hiyo. Vilevile mkoani humo, jeshi la Iraq limewashambulia na kuwakamata viongozi watatu wa IS katika eneo lililo karibu na kijiji cha mkheisa, ambao ni hatari na muhimu katika muundo wa kundi hilo mkoani Diyala.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |