Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistan imemwita naibu kamishna wa ngazi ya juu wa India na kuionya India dhidi ya mipango yake inayoshukiwa ya kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya Pakistan katika siku zijazo. Onyo hilo limekuja baada ya waziri wa mambo ya nje wa Pakistan Shah Mahmood Qureshi kusema kwenye mkutano na waandishi wa habari kuwa kuna taarifa ya kijasusi ya kuaminika kuwa India inaandaa mpango mpya wa kuishambulia Pakistan, na ameongeza kuwa kama India inatekeleza mpango huo itaathiri vibaya amani na utulivu wa kanda hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |