Matumaini ya Kenya kuwa na timu mbili kwenye michuano ya raga ya dunia yamezimwa baada ya timu ya taifa ya raga ya Kenya (Lionesses) kuzidiwa ujanja na Brazil katika nusu-fainali kwa alama 17-5 mjini Hong Kong mnamo Ijumaa katika mechi za kufuzu kushiriki raga ya dunia ya wanawake ya msimu 2019-2020.
Lionesses, ambayo ilizimwa na Afrika Kusini katika nusu fainali ya mchujo wa mwaka 2018 mjini Hong Kong, iliingia mechi ya Brazil ikiwa na motisha ya kuipepeta Uganda 24-0, Hong Kong 36-5 na Papua New Guinea 20-10 katika mechi za kundi B na kuizaba Argentina 17-15 katika robo-fainali. Fainali ya michuano hiyo itazikutanisha timu za Brazil na Scotland.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |