Wakiwa nyumbani jijini Nairobi, timu ya Gor Mahia imekubali kichapo cha jumla ya magoli 2-0 toka kwa Berkane ya Morocco katika mchezo wa robo fainali ya kombe la shirikisho barani Afrika.
Gor Mahia sasa wanatakiwa kuwafunga wapinzani wao hawa jumla ya mabao 3-0 katika mchezo wa marudiano utakaopigwa nchini Morocco ili waweze kutinga nusu fainali.
Nayo Nkana Red Devils ya Zambia, imeibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya CS Sfaxien mchezo uliopigwa katika uwanja wa Nkana mjini Kitwe Zambia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |