Shirika la Fedha la Kimataifa IMF limeshusha makadirio ya ukuaji wa uchumi wa dunia kwa mwaka 2019 hadi asilimia 3.3 katika ripoti yake mpya ya Mustakbali wa Uchumi wa Dunia, WEO. IMF imesema uchumi wa dunia unakabiliwa na hatari za kushuka zinazotokana na sintofahamu katika mivutano ya kibiashara inayoendelea, pamoja na sababu nyingine za nchi na sekta maalumu. Makadirio hayo ya asilimia 3.3 kwa mwaka 2019 ni asilimia 0.3 chini kuliko kiwango cha mwaka jana, lakini yatakuwa asilimia 3.6 kwa mwaka 2020.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |