Kampeni hiyo ya elimu kwa umma imefanyika katika maeneo mbalimbali zikiwamo shule za msingi na sekondari, masoko, stendi, minadani na maeneo mengine ya wazi ambapo wananchi walijitokeza kupata elimu na ufahamu wa masuala mbalimbali yahusuyo ubora wa bidhaa.
Ofisa Masoko Mwandamizi, Gladness Kaseka, aliwakumbusha wananchi wote kuwa vita ya bidhaa hafifu sio ya TBS pekee bali ni ya Taifa kwa ujumla.
Aliwasisitiza wananchi kuendelea kutoa taarifa kupitia mawasiliano waliyopewa pale wanapogundua uwapo wa bidhaa hafifu katika soko.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |