Jumuiya ya Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) imehimiza nchi wanachama wake kuchukua hatua kulinda usalama wa vyakula ili kuongeza biashara ya ndani.
Ofisa mkuu wa maendeleo ya sekta binafsi, Innocent Makwiramiti amesema, COMESA inajitahidi kuongeza uwezo wa sekta binafsi na za umma za nchi wanachama wake katika kuhakikisha usafi wa vyakula na mazao ya kilimo ili kuwezesha bidhaa zao kuingia kwenye soko la kikanda na la kimataifa.
Bw. Makwiramiti pia amesema, kiwango cha chini cha usalama wa vyakula ni sababu muhimu ya kuzuia maendeleo ya eneo la biashara huria la Afrika, AfCFTA.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |