• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wakulima asilimia 72 wamesajiliwa

    (GMT+08:00) 2019-04-15 20:18:11
    Waziri wa Kilimo nchini Tanzania Bw Japhet Hasunga amesema ni asilimia 72 ya wakulima wa mazao nane ya biashara wameshasajiliwa ili waweze kupatiwa vitambulisho bure. Alisema hayo baada ya kupokea vifaa mbalimbali zikiwamo `tablets' 50 zitakazosaidia kusajili wakulima nchini humo.

    Alisema kuna tatizo kubwa la takwimu za wakulima na kwamba kutokana na hali hiyo, wizara imeanza kuwasajili ili mazao wanayolima yatambulike, kwa ukubwa gani na wapo kwenye maeneo gani.

    Alitaja mazao hayo kuwa ni pamba, miwa, korosho, kahawa, chai, pareto, alizeti na michikichi na hadi Machi 31, mwaka huu, wameshaandikishwa wakulima 1,274,337 sawa na asilimia 72.

    Alisema lengo ni kuwafikia wakulima milioni 1.7 na kuzitaka bodi za mazao hayo zikamilishe kazidata hiyo ili kujua wako wapi.

    Hasunga alisema kwa sasa kuna mashamba 134 makubwa ya kahawa, pareto, mkonge, chai, pamba na korosho na alitaka kujua kama kuna mazao mengine ambayo yana mashamba makubwa, hivyo akahimiza kukamilisha usajili ili kujua mashamba hayo.

    Alilishukuru Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), kwa kutoa vifaa hivyo kwa ajili ya kusaidia usajili wa wakulima nchini humo kitengo ambacho kitaongeza ubora na uhakika wakulima walipo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako