Polisi nchini Afrika Kusini watateketeza bunduki haramu elfu 30 zilizokamatwa baada ya kutumiwa kufanya uhalifu, ambazo kesi zake zimeshahitimishwa. Msemaji wa polisi Vish Naidoo amesema tangu uharibifu kama huo kufanyika kote nchini mwaka 2016, polisi wamekamata idadi kubwa ya silaha haramu katika operesheni zilizoratibiwa na kusababisha malimbikizo katika maghala ya kuhifadhi silaha. Ameongeza kuwa wataendelea kupambana na kuongezeka kwa silaha na risasi haramu ambazo zinatishia usalama wa umma.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |