Timu ya soka ya vijana wenye umri wa miaka chini ya 17 ya Tanzania (Serengeti Boys) imeendelea kufanya vibaya kwenye fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa vijana AFCON U-17 baada ya jana kwa mara nyingine kuchapwa bao 3-0 na timu ya vijana ya Uganda uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kocha wa Serengeti Boys amezungumza na Global TV na kutoa utetezi wake baada ya kupigwa bao 9 ndani ya dakika 180.
Insert: Kocha wa Serengeti Boys
Sasa Serengeti Boys itahitaji miujiza kuweza kuingia Nusu Fainali iwapo itaifunga Angola kuanzia 3-0 na Uganda itafungwa na Nigeria si chini ya 3-0 kwenye mechi za mwisho ili ifuzu kwa wastani wa mabao. Mechi za mwisho za Kundi A zitachezwa Aprili 20 Serengeti Boys ikimenyana na Angola Uwanja wa Taifa na Nigeria na Uganda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |