Kwa sasa, kuna mazungumzo kati ya wafanyibiashara wa binafsi na usimamizi wa jiji la Kigali kuona ni vipi siku hii itatumiwa kuinua uchumi wa Rwanda. Endapo hili litaafikiwa, basi siku hii ya kutoruhusu magari kuingia jijini Kigali, itakuwa ikitumika kunadi na kutangaza bidhaa ambazo zimetengenezewa nchini Rwanda. Watakao pewa ipao mbele ni vijana wajasiriamali wa kiwango cha chini na kati. Baadhi ya bidhaa zitakazouzwa ni sanaa,mapambo,mavazi, viatu na vinywaji vyeney asili ya Rwanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |