Man City imeibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Manchester United, Manchester City sasa inafikisha alama 89 baada ya ushindi huo katika michezo 35 huku Man United ikisalia na alama zake 64 baada ya kucheza mechi 34 na kuwa katika nafasi ya sita ya ligi hiyo.
Mchezo mwingine ulikuwa kati ya washika bunduki wa jiji la London Arsenal walipokubali kipigo cha mbwa mwizi cha 3-1 toka kwa Wolverhampton Wanderers mchezo uliopigwa uwanja wa Molineux. Mabao ya Wolves yalipachikwa na Ruben Neves dakika ya 28, Matt Doherty dakika ya 37 na Diogo Jota dakika ya 45. Huku goli la kufuta machozi la Arsenal limefungwa na Sokratis Papa stathopoulos dakika ya 80.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |