• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania iko kwenye hatua za kuridhia biashara huru Afrika

    (GMT+08:00) 2019-04-25 20:44:45
    Tanzania ipo kwenye hatua za kuridhia biashara huru kwa wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) unaoundwa na nchi 55.

    Akizungumza jana, Afisa Biashara, Thomas Mcharo, ambaye ni Mwakilishi wa Mkurugenzi Msaidizi Idara ya mtangamano wa biashara Wizara ya Viwanda na Biashara, alieleza kuwa lengo la kuanzishwa biashara ya pamoja kwa jumuiya hizo ni kukuza uchumi.

    Alisema biashara hiyo imegawanyika katika hatua tatu, ambayo ni asilimia 90 ya bidhaa zinazopatikana kwa wanachama wa jumuiya hiyo kutotozwa ushuru katika vituo vya forodha, asilimia tatu watalipia kwa awamu na asilimia saba hazitofunguliwa.

    Mcharo alisema biashara huru itaisaidia Tanzania kutokana na mkakati wake wa kuingia katika uchumi wa kati kupitia ujenzi wa viwanda, kwa kuwa viwanda vitazalisha na kutakuwa na masoko ya kutosha.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako