Mshambuliaji wa Paris St-Germain, Neymar amekutana na rungu la shirikisho la soka ulaya (UEFA) na kufungiwa mechi tatu za msimu ujao za hatua ya awali ya ligi ya mabingwa.
Katika taarifa yake UEFA imesema, Neymar aliwadhihaki waamuzi kupitia akaunti yake ya Instagram baada ya timu yao kutolewa nje ya michuano hiyo na Manchester United.
Mbrazil huyo alimdhihaki mwamuzi Damir Skomina ambaye alilazimika kutumia usaidizi wa video (VAR) kutoa penalti iliyowamaliza PSG kwenye michuano hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |