Kamati ya utendaji ya shirikisho la soka la DRC (FECOFA) limeeleza kuhusu kuondolewa kwenye michuano hiyo kwa timu ya taifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 23 (Leopards) katika michuano ya mataifa ya Afrika ya wachezaji CAF 2019.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mwishoni mwa wiki, shirikisho la soka Afrika liliiondoa timu hiyo kufuatia kosa la kiutawala lililofanywa na shirikisho la soka DRC kumruhusu mchezaji Arsène Zola kushiriki michuano hiyo ingali umri wake haumruhusu kushiriki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |