Rekodi ya ushindi imeendelea kuibeba Yanga mbele ya Azam FC katika michuano ya ligi kuu Tanzania bara, mchezo ulipigwa jana uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Yanga ikiwa ugenini imefanikiwa kuondoka na alama tatu muhimu baada ya ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Mrisho Ngassa aliyetumia vyema pasi ya Ibrahim Ajib, ushindi huo unakuwa ushindi wa 8 wa Yanga dhidi ya Azam wakiwa wamekutana mara 21, sare zikiwa 7 na Yanga kupoteza mara 6 tu dhidi ya Azam.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |