Idara ya uhamiaji ya taifa ya China imesema kuwa, sikukuu inayokaribia ya tarehe Mosi Mei nchini China inatarajiwa kushuhudia wastani wa watalii milioni 2.2 wanaotoka na kuingia ikiwa ni wachina pamoja na wageni, likiwa ni ongezeko la asilimia 5.9 ikilinganishwa na mwaka jana.
Mwaka huu mapumziko ya mwaka huu yanaanzia tarehe I hadi tarehe 4 Mei, ikiwa ni siku nyingi kuliko miaka ya nyuma, na kuruhusu watu kufanya safari ndefu, na kufanya idadi ya wasafiri kwenye miji kama Beijing na Shanghai itaongezeka
Idara ya uhamiaji ya taifa imezitaka mamlaka zinazosimamia mipaka kutoa taarifa kwa wakati, ili kuhakikisha wasafiri wanasafiri vizuri na watalii kuwa na usalama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |